Kumbukeni Kujiandaa Kukabiliana na Ukame Terrat Simanjiro

Jamii ya wafugaji wa kijiji cha Terrat, Wilaya ya Simanjiro, inakumbushwa kutumia vizuri msimu huu wa mvua kuandaa malisho kwa ajili ya mifugo ili kuepuka hasara katika kipindi kijacho cha kiangazi.

Mwaka uliopita wafugaji wengi walipoteza mifugo yao huku wengine wakitumia gharama kubwa kunusuru mifugo kutokana na ukosefu wa malisho na maji. Mfugaji Daniel Leboi Ngoira anakumbusha uzoefu wake akisema:

“Ilinilazimu kutumia gharama kubwa kuhamisha mifugo, kukodi trekta na boza kwa ajili ya maji, na kununua chakula cha mifugo badala ya kutumia fedha hizo kununulia chakula cha familia. Tusipojiandaa mapema, tutaingia tena gharama hizi kubwa.”

Aidha, Mwenyekiti wa kijiji cha Terrat, Kone P. Medukenya, anawakumbusha wakazi wa kijiji hicho kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi, kulinda maeneo maalumu yaliyotengwa kwa ajili ya malisho, na kushiriki kikamilifu katika mashamba darasa ya malisho yanayosimamiwa kwa ushirikiano na shirika la TNC kupitia mradi wa Green Kilimo.

“Huu ndiyo wakati wa kuhakikisha maeneo yetu ya malisho yanalindwa, kuhifadhi mbegu za majani, na kuhakikisha tunafuata utaratibu wa kulisha mifugo ili kipindi cha ukame kisitukute hatuna maandalizi,” amesema Medukenya.

Kumbukeni, maandalizi ya sasa yatasaidia kupunguza athari za ukame na hasara kwa mifugo yenu msimu ujao wa kiangazi.

Related Posts

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limefanya ukaguzi maalumu wa mabasi ya abiria ili kudhibiti ajali kutokana na ongezeko la wasafiri kipindi cha likizo za shule. Madereva wamehimizwa kuzingatia sheria…

Continue reading
Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Zaidi ya madereva 800 wa magari ya utalii mkoani Arusha wamepatiwa mafunzo maalumu yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, ikiwa ni maandalizi ya msimu wa utalii (high…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe

Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe
Enable Notifications OK No thanks