Mama Lishe Arusha Wanufaika na Majiko ya Gesi Safi

Na nyangusi Ole Sang’ida

Wafanyabiashara wadogo maarufu kama Mama Lishe na Baba Lishe katika Halmashauri ya Wilaya ya Arusha wamepokea kwa furaha majiko ya gesi yaliyotolewa na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ili kuboresha shughuli zao za upishi pamoja na kuhifadhi mazingira.

Katika zoezi la kugawa majiko hayo lililofanyika jana, Mkurugenzi wa Halmashauri ya Arusha, Bw. Seleman Msumi amesema majiko hayo 50 ni utekelezaji wa ajenda ya Rais Samia katika kuhakikisha Watanzania wanaachana na matumizi ya kuni na mkaa ambayo husababisha uharibifu mkubwa wa mazingira.

Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo, Bw. Ojungu Salekwa amesema zoezi hilo ni awamu ya kwanza, likiwa na lengo la kuhifadhi mazingira, kulinda vyanzo vya maji na kupunguza athari za kiafya zinazotokana na moshi wa kuni.

Akizungumza kwa niaba ya Mama Lishe, Neema Burra kutoka Kata ya Oljoro amesema wamekuwa wakipata changamoto kubwa ikiwemo kuumwa macho kutokana na moshi wa kuni na kwamba matumizi ya gesi yataokoa muda na kuwawezesha kufanya biashara kwa ufanisi zaidi.

“Namshukuru sana Rais Samia kwa kutupatia gesi, imeniondolea madhara ya kiafya kama maumivu ya macho yanayosababishwa na moshi wa kuni. Gesi ni safi kwa afya, mazingira na biashara yetu,” amesema Neema.

Zoezi hili limetajwa kuwa litasaidia kupunguza ukataji miti, kulinda mazingira na kuinua uchumi wa wafanyabiashara wadogo katika halmashauri hiyo.

Kwa habari zaidi tembelea tovuti yetu: www.ors-radio.co.tz

Related Posts

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

Continue reading
Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
Enable Notifications OK No thanks