Kumbukeni Kujiandaa Kukabiliana na Ukame Terrat Simanjiro

Jamii ya wafugaji wa kijiji cha Terrat, Wilaya ya Simanjiro, inakumbushwa kutumia vizuri msimu huu wa mvua kuandaa malisho kwa ajili ya mifugo ili kuepuka hasara katika kipindi kijacho cha kiangazi.

Mwaka uliopita wafugaji wengi walipoteza mifugo yao huku wengine wakitumia gharama kubwa kunusuru mifugo kutokana na ukosefu wa malisho na maji. Mfugaji Daniel Leboi Ngoira anakumbusha uzoefu wake akisema:

“Ilinilazimu kutumia gharama kubwa kuhamisha mifugo, kukodi trekta na boza kwa ajili ya maji, na kununua chakula cha mifugo badala ya kutumia fedha hizo kununulia chakula cha familia. Tusipojiandaa mapema, tutaingia tena gharama hizi kubwa.”

Aidha, Mwenyekiti wa kijiji cha Terrat, Kone P. Medukenya, anawakumbusha wakazi wa kijiji hicho kuzingatia mpango wa matumizi bora ya ardhi, kulinda maeneo maalumu yaliyotengwa kwa ajili ya malisho, na kushiriki kikamilifu katika mashamba darasa ya malisho yanayosimamiwa kwa ushirikiano na shirika la TNC kupitia mradi wa Green Kilimo.

“Huu ndiyo wakati wa kuhakikisha maeneo yetu ya malisho yanalindwa, kuhifadhi mbegu za majani, na kuhakikisha tunafuata utaratibu wa kulisha mifugo ili kipindi cha ukame kisitukute hatuna maandalizi,” amesema Medukenya.

Kumbukeni, maandalizi ya sasa yatasaidia kupunguza athari za ukame na hasara kwa mifugo yenu msimu ujao wa kiangazi.

Related Posts

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

Continue reading
Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
Enable Notifications OK No thanks