Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana mmoja aitwaye Joseph Gadiel mkazi wa kitongoji cha Kimelok, kijiji cha Ngiresi wilayani Arusha ameuawa kwa kuchomwa kisu baada ya kutokea ugomvi baina yake na kijana mwingine aliyetambulika kwa jina la William Mungas Sandile, mkazi wa kitongoji cha Olturoto.

Akizungumzia tukio hilo, Mwenyekiti wa kijiji cha Ngiresi, Jonas Lemeitei amesema tukio hilo limetokea baada ya vijana hao kutokea kwenye baa ambapo ugomvi uliibuka na kupelekea Joseph kuchomwa kisu na kufariki dunia alipofikishwa hospitalini kwa matibabu.

Ameongeza kuwa tayari tukio hilo limeripotiwa Polisi, na uchunguzi unaendelea ili kubaini chanzo halisi cha ugomvi huo.

Kwa upande wake, Aminiel Simon, mkazi wa Olturoto, amesema alishuhudia tukio hilo na kwamba vijana hao wenye hasira walikuwa wakitafuta kumdhuru mtuhumiwa lakini walipomkosa wakaamua kuchoma nyumba yake.

Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha bado hajatoa taarifa rasmi juu ya tukio hili. Polisi wanaendelea kumsaka mtuhumiwa ambaye ametoroka baada ya kufanya tukio hilo.

Wananchi wametakiwa kuwa watulivu na kuacha kujichukulia sheria mikononi, badala yake kuruhusu vyombo husika kuchukua hatua za kisheria.

Related Posts

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

Continue reading
Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
Enable Notifications OK No thanks