Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Mbunge wa Monduli Fred Lowassa akiwa katika sherehe ya kimila iliyofanyika kata ya Meserani Monduli tarehe 25/05/2025.

“Serikali yetu haiwezi kufurahia kuona jamii yetu inahangaika na masuala ya malisho. Nimejiridhisha kwamba maeneo yetu yataendelea kutumika kwa malisho na mafunzo ya kijeshi,” alisema Lowassa.

Mbunge wa Jimbo la Monduli, Mhe. Fredrick Lowassa amewataka wananchi wa jamii ya Maa kuwa na umoja na uangalifu dhidi ya watu wanaotaka kuwagombanisha na serikali kwa malengo yao binafsi.

Akizungumza kwenye sherehe ya vijana maarufu kama “Engipaata oo Irmegoliki” iliyofanyika Kata ya Meserani Mei 25, 2025, Mhe. Lowassa amesema kumekuwa na tabia ya baadhi ya watu aliowaita “madalali” kuitumia jamii hiyo kuleta migogoro ili wao wapate manufaa.

Amesema serikali ya Chama cha Mapinduzi chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ni serikali sikivu na yenye nia njema kwa jamii ya Maa, hasa katika kulinda maeneo yao ya malisho.

“Serikali yetu haiwezi kufurahia kuona jamii yetu inahangaika na masuala ya malisho. Nimemtafuta Waziri wa Ulinzi na nimejiridhisha kwamba maeneo yetu yataendelea kutumika kwa malisho na mafunzo ya kijeshi,” alisema Lowassa.

Aidha, Lowassa amewataka wananchi hao kuhakikisha wanaendelea kuiunga mkono serikali ya Chama cha Mapinduzi ili kulinda maslahi yao na kuhakikisha maendeleo endelevu yanafikiwa katika jamii ya Maa.

Amewataka wananchi kuwa watulivu, wenye umoja na kuendelea kushirikiana na serikali katika kusimamia masuala yao muhimu bila kudanganywa na watu wenye nia ovu.

  • Related Posts

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

    Continue reading
    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

    Continue reading

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
    Enable Notifications OK No thanks