Bei ya mahindi katika soko la Terrat

Wakaazi wa kijiji cha Terrat wilaya ya Simanjiro wamelalamikia hali ya mfumuko wa bei ya mahindi ulivyongezeka kwa zaidi kutoka shilingi elfu 7,000 hadi shilingi elfu 15,000.

Jamii ya wafugaji wa kijiji cha Terrat, wilayani Simanjiro, mkoa wa Manyara, wanakabiliana na changamoto kubwa kutokana na kupanda kwa bei ya mahindi sokoni. Mahindi, ambayo ni chakula kikuu kwa familia nyingi za wafugaji, yamekuwa ghali zaidi, hali inayoongeza mzigo wa maisha.

Kwa mujibu wa wakazi wa Terrat, bei ya mahindi kwa sasa imepanda kwa zaidi ya asilimia 50 katika miezi michache iliyopita. Wakati huo huo, mifugo ambayo ndiyo kitega uchumi kikuu kwa jamii ya wafugaji, inapoteza thamani sokoni kutokana na athari za ukame, hali inayosababisha mifugo kuwa dhaifu na kushindwa kupata soko la uhakika.

Takwimu kutoka soko la Terrat zinaonyesha kuwa kwa sasa, bei ya debe moja la mahindi imepanda kutoka TZS 25,000 hadi kufikia TZS 40,000, ongezeko ambalo ni changamoto kubwa kwa familia zinazotegemea mifugo kama chanzo kikuu cha kipato. Wafugaji wengi wanapambana kupata fedha za kununua chakula huku mifugo yao ikiendelea kupoteza thamani.

Related Posts

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

Serikali za vijiji katika Tarafa ya Terrat, wilayani Simanjiro, zimetakiwa kuwa na ushirikiano mzuri na wawekezaji waliopo kwenye maeneo yao kwa kuwaalika na kuwatembelea ili kujenga mahusiano mazuri na kushirikiana…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

Maji Safi na Salama ni Yapi?

Maji Safi na Salama ni Yapi?

Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja

Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja
Enable Notifications OK No thanks