Ushiriki wa Wanawake Katika Mikutano ya Maendeleo Kijijini Loswaki Wajadiliwa

#Habari Katika kijiji cha Loswaki, kilichopo wilayani Simanjiro, ushiriki wa wanawake katika mikutano ya kijamii umeendelea kuwa mada ya mjadala wa maendeleo. Wanawake kama Winifrida Amos, mkazi wa kijiji hicho, wanasema kuwa kushiriki katika mikutano ni fursa ya kipekee ya kuhakikisha masuala yanayohusu wanawake yanajadiliwa ipasavyo na kupata ufumbuzi.

“Ninapenda kushiriki katika mikutano kwa sababu unakuta mambo yanayowahusu wanawake hayatetewi” anasema Winifrida. Hata hivyo, anasisitiza kuwa mila na desturi zisizofaa zinazomkandamiza mwanamke ni changamoto kubwa katika jamii ya Kimasai.

Changamoto za Ushiriki wa Wanawake

Moses Lukumay, Mwenyekiti wa kijiji cha Loswaki, anakiri kuwa ushiriki wa wanawake katika mikutano bado ni wa kiwango cha chini licha ya kuwepo kwa juhudi za kuhimiza wanawake kushiriki. Anasema kuwa wanawake wanaoshiriki, kama Winifrida Amos, mara nyingi wanatoa maoni yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya kijiji.

Kwa upande wake, Afisa Tarafa wa Terrat, Lekshon Kiruswa, anasema kuwa changamoto ya ushiriki wa wanawake haipo kijijini Loswaki pekee bali ni changamoto inayojitokeza katika tarafa nzima ya Terrat. Anasema jitihada za kuwahamasisha wanawake kushiriki katika mijadala ya kijamii zinaendelea kufanyika.

“Muamko wa wanawake kushiriki katika mijadala bado upo chini kwenye tarafa yetu” anasema Kiruswa.

Juhudi za Kukuza Ushiriki wa Wanawake

Ili kuboresha ushiriki wa wanawake, viongozi wa kijiji na tarafa wanapendekeza kuondoa vizuizi vya kijamii vinavyowazuia wanawake kushiriki kikamilifu, ikiwa ni pamoja na elimu ya umuhimu wa usawa wa kijinsia na kuhamasisha jamii kuachana na mila kandamizi.

  • Related Posts

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

    Continue reading
    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

    Continue reading

    One thought on “Ushiriki wa Wanawake Katika Mikutano ya Maendeleo Kijijini Loswaki Wajadiliwa

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
    Enable Notifications OK No thanks