Bei ya mahindi katika soko la Terrat

Wakaazi wa kijiji cha Terrat wilaya ya Simanjiro wamelalamikia hali ya mfumuko wa bei ya mahindi ulivyongezeka kwa zaidi kutoka shilingi elfu 7,000 hadi shilingi elfu 15,000.

Jamii ya wafugaji wa kijiji cha Terrat, wilayani Simanjiro, mkoa wa Manyara, wanakabiliana na changamoto kubwa kutokana na kupanda kwa bei ya mahindi sokoni. Mahindi, ambayo ni chakula kikuu kwa familia nyingi za wafugaji, yamekuwa ghali zaidi, hali inayoongeza mzigo wa maisha.

Kwa mujibu wa wakazi wa Terrat, bei ya mahindi kwa sasa imepanda kwa zaidi ya asilimia 50 katika miezi michache iliyopita. Wakati huo huo, mifugo ambayo ndiyo kitega uchumi kikuu kwa jamii ya wafugaji, inapoteza thamani sokoni kutokana na athari za ukame, hali inayosababisha mifugo kuwa dhaifu na kushindwa kupata soko la uhakika.

Takwimu kutoka soko la Terrat zinaonyesha kuwa kwa sasa, bei ya debe moja la mahindi imepanda kutoka TZS 25,000 hadi kufikia TZS 40,000, ongezeko ambalo ni changamoto kubwa kwa familia zinazotegemea mifugo kama chanzo kikuu cha kipato. Wafugaji wengi wanapambana kupata fedha za kununua chakula huku mifugo yao ikiendelea kupoteza thamani.

Related Posts

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

Continue reading
Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
Enable Notifications OK No thanks