Ushiriki wa Wanawake Katika Mikutano ya Maendeleo Kijijini Loswaki Wajadiliwa

#Habari Katika kijiji cha Loswaki, kilichopo wilayani Simanjiro, ushiriki wa wanawake katika mikutano ya kijamii umeendelea kuwa mada ya mjadala wa maendeleo. Wanawake kama Winifrida Amos, mkazi wa kijiji hicho, wanasema kuwa kushiriki katika mikutano ni fursa ya kipekee ya kuhakikisha masuala yanayohusu wanawake yanajadiliwa ipasavyo na kupata ufumbuzi.

“Ninapenda kushiriki katika mikutano kwa sababu unakuta mambo yanayowahusu wanawake hayatetewi” anasema Winifrida. Hata hivyo, anasisitiza kuwa mila na desturi zisizofaa zinazomkandamiza mwanamke ni changamoto kubwa katika jamii ya Kimasai.

Changamoto za Ushiriki wa Wanawake

Moses Lukumay, Mwenyekiti wa kijiji cha Loswaki, anakiri kuwa ushiriki wa wanawake katika mikutano bado ni wa kiwango cha chini licha ya kuwepo kwa juhudi za kuhimiza wanawake kushiriki. Anasema kuwa wanawake wanaoshiriki, kama Winifrida Amos, mara nyingi wanatoa maoni yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya kijiji.

Kwa upande wake, Afisa Tarafa wa Terrat, Lekshon Kiruswa, anasema kuwa changamoto ya ushiriki wa wanawake haipo kijijini Loswaki pekee bali ni changamoto inayojitokeza katika tarafa nzima ya Terrat. Anasema jitihada za kuwahamasisha wanawake kushiriki katika mijadala ya kijamii zinaendelea kufanyika.

“Muamko wa wanawake kushiriki katika mijadala bado upo chini kwenye tarafa yetu” anasema Kiruswa.

Juhudi za Kukuza Ushiriki wa Wanawake

Ili kuboresha ushiriki wa wanawake, viongozi wa kijiji na tarafa wanapendekeza kuondoa vizuizi vya kijamii vinavyowazuia wanawake kushiriki kikamilifu, ikiwa ni pamoja na elimu ya umuhimu wa usawa wa kijinsia na kuhamasisha jamii kuachana na mila kandamizi.

  • Related Posts

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    Serikali za vijiji katika Tarafa ya Terrat, wilayani Simanjiro, zimetakiwa kuwa na ushirikiano mzuri na wawekezaji waliopo kwenye maeneo yao kwa kuwaalika na kuwatembelea ili kujenga mahusiano mazuri na kushirikiana…

    Continue reading

    One thought on “Ushiriki wa Wanawake Katika Mikutano ya Maendeleo Kijijini Loswaki Wajadiliwa

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    Maji Safi na Salama ni Yapi?

    Maji Safi na Salama ni Yapi?

    Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

    Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

    Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

    Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

    Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

    Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

    Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja

    Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja
    Enable Notifications OK No thanks