Ushiriki wa Wanawake Katika Mikutano ya Maendeleo Kijijini Loswaki Wajadiliwa

#Habari Katika kijiji cha Loswaki, kilichopo wilayani Simanjiro, ushiriki wa wanawake katika mikutano ya kijamii umeendelea kuwa mada ya mjadala wa maendeleo. Wanawake kama Winifrida Amos, mkazi wa kijiji hicho, wanasema kuwa kushiriki katika mikutano ni fursa ya kipekee ya kuhakikisha masuala yanayohusu wanawake yanajadiliwa ipasavyo na kupata ufumbuzi.

“Ninapenda kushiriki katika mikutano kwa sababu unakuta mambo yanayowahusu wanawake hayatetewi” anasema Winifrida. Hata hivyo, anasisitiza kuwa mila na desturi zisizofaa zinazomkandamiza mwanamke ni changamoto kubwa katika jamii ya Kimasai.

Changamoto za Ushiriki wa Wanawake

Moses Lukumay, Mwenyekiti wa kijiji cha Loswaki, anakiri kuwa ushiriki wa wanawake katika mikutano bado ni wa kiwango cha chini licha ya kuwepo kwa juhudi za kuhimiza wanawake kushiriki. Anasema kuwa wanawake wanaoshiriki, kama Winifrida Amos, mara nyingi wanatoa maoni yenye mchango mkubwa katika maendeleo ya kijiji.

Kwa upande wake, Afisa Tarafa wa Terrat, Lekshon Kiruswa, anasema kuwa changamoto ya ushiriki wa wanawake haipo kijijini Loswaki pekee bali ni changamoto inayojitokeza katika tarafa nzima ya Terrat. Anasema jitihada za kuwahamasisha wanawake kushiriki katika mijadala ya kijamii zinaendelea kufanyika.

“Muamko wa wanawake kushiriki katika mijadala bado upo chini kwenye tarafa yetu” anasema Kiruswa.

Juhudi za Kukuza Ushiriki wa Wanawake

Ili kuboresha ushiriki wa wanawake, viongozi wa kijiji na tarafa wanapendekeza kuondoa vizuizi vya kijamii vinavyowazuia wanawake kushiriki kikamilifu, ikiwa ni pamoja na elimu ya umuhimu wa usawa wa kijinsia na kuhamasisha jamii kuachana na mila kandamizi.

  • Related Posts

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limefanya ukaguzi maalumu wa mabasi ya abiria ili kudhibiti ajali kutokana na ongezeko la wasafiri kipindi cha likizo za shule. Madereva wamehimizwa kuzingatia sheria…

    Continue reading
    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Zaidi ya madereva 800 wa magari ya utalii mkoani Arusha wamepatiwa mafunzo maalumu yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, ikiwa ni maandalizi ya msimu wa utalii (high…

    Continue reading

    One thought on “Ushiriki wa Wanawake Katika Mikutano ya Maendeleo Kijijini Loswaki Wajadiliwa

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

    Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

    Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe

    Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe
    Enable Notifications OK No thanks