Recho Thomas: Binti Shujaa Anayepaza Sauti Dhidi ya Ukeketaji katika Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia

Jifunze simulizi ya Recho Thomas, binti wa jamii ya Wamasai aliyeepuka ukeketaji na sasa ni sauti ya mabadiliko. Soma na Sikiliza jinsi alivyoshinda mila potofu na juhudi za kumaliza ukatili huu.

Katika kipindi hiki cha likizo ya Desemba, jamii nyingi za kifugaji hufanya sherehe kubwa, ikiwemo ukeketaji wa mabinti kama sehemu ya mila na tamaduni za zamani. Lakini simulizi ya Recho Thomas ni ya kipekee. Akiwa binti wa jamii ya Wamasai, Recho alikataa kufuata mila hii na sasa anapaza sauti kwa niaba ya wasichana wengine walio hatarini.

Changamoto Anazopitia Wasichana Wasio Keketwa
Kwa mujibu wa ripoti ya Demographic and Health Survey ya 2015-2016, asilimia 58 ya wanawake wenye umri wa miaka 15-49 katika Mkoa wa Manyara wamefanyiwa ukeketaji, hali inayoonyesha ukubwa wa tatizo. Lakini kwa wale waliokataa mila hii, maisha si rahisi. Recho anasema:
“Mara nyingi unakutana na unyanyapaa kutoka kwa jamii, familia, na hata marafiki. Lakini nilijua uamuzi wangu ulikuwa sahihi.”

Kwa msaada wa mashirika kama Pastoral Women Council (PWC),na Taasisi za Dini Recho alipata ujasiri wa kusimama imara dhidi ya shinikizo la jamii. Sasa, anahamasisha wasichana wengine kupinga ukatili huu kupitia majukwaa ya kijamii na semina za uhamasishaji.

Nini Kimefanyika Kupinga Ukeketaji?

Afisa Uga wa PWC, Grace Mbario Tayayi, anasema:
“Elimu ni silaha kubwa. Tunawahamasisha wazazi na viongozi wa kijamii kubadilisha mitazamo yao kuhusu mila hizi. Hali inabadilika, ingawa bado kuna changamoto.”

  • Related Posts

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    Serikali za vijiji katika Tarafa ya Terrat, wilayani Simanjiro, zimetakiwa kuwa na ushirikiano mzuri na wawekezaji waliopo kwenye maeneo yao kwa kuwaalika na kuwatembelea ili kujenga mahusiano mazuri na kushirikiana…

    Continue reading

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    Maji Safi na Salama ni Yapi?

    Maji Safi na Salama ni Yapi?

    Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

    Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

    Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

    Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

    Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

    Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

    Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja

    Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja
    Enable Notifications OK No thanks