Recho Thomas: Binti Shujaa Anayepaza Sauti Dhidi ya Ukeketaji katika Siku 16 za Kupinga Ukatili wa Kijinsia

Jifunze simulizi ya Recho Thomas, binti wa jamii ya Wamasai aliyeepuka ukeketaji na sasa ni sauti ya mabadiliko. Soma na Sikiliza jinsi alivyoshinda mila potofu na juhudi za kumaliza ukatili huu.

Katika kipindi hiki cha likizo ya Desemba, jamii nyingi za kifugaji hufanya sherehe kubwa, ikiwemo ukeketaji wa mabinti kama sehemu ya mila na tamaduni za zamani. Lakini simulizi ya Recho Thomas ni ya kipekee. Akiwa binti wa jamii ya Wamasai, Recho alikataa kufuata mila hii na sasa anapaza sauti kwa niaba ya wasichana wengine walio hatarini.

Changamoto Anazopitia Wasichana Wasio Keketwa
Kwa mujibu wa ripoti ya Demographic and Health Survey ya 2015-2016, asilimia 58 ya wanawake wenye umri wa miaka 15-49 katika Mkoa wa Manyara wamefanyiwa ukeketaji, hali inayoonyesha ukubwa wa tatizo. Lakini kwa wale waliokataa mila hii, maisha si rahisi. Recho anasema:
“Mara nyingi unakutana na unyanyapaa kutoka kwa jamii, familia, na hata marafiki. Lakini nilijua uamuzi wangu ulikuwa sahihi.”

Kwa msaada wa mashirika kama Pastoral Women Council (PWC),na Taasisi za Dini Recho alipata ujasiri wa kusimama imara dhidi ya shinikizo la jamii. Sasa, anahamasisha wasichana wengine kupinga ukatili huu kupitia majukwaa ya kijamii na semina za uhamasishaji.

Nini Kimefanyika Kupinga Ukeketaji?

Afisa Uga wa PWC, Grace Mbario Tayayi, anasema:
“Elimu ni silaha kubwa. Tunawahamasisha wazazi na viongozi wa kijamii kubadilisha mitazamo yao kuhusu mila hizi. Hali inabadilika, ingawa bado kuna changamoto.”

  • Related Posts

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

    Continue reading
    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

    Continue reading

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
    Enable Notifications OK No thanks