Kaya 22 Zenye Watu 96 Zapokelewa Rasmi Msomera Kutoka Ngorongoro

Jumla ya kaya 22 zenye watu 96 na mifugo 196 zilizohama kwa hiari kutoka ndani ya Hifadhi ya Ngorongoro zimepokelewa rasmi katika Kijiji cha Msomera, Wilayani Handeni. Kaya hizo zimekabidhiwa makazi mapya, mashamba, na maeneo ya ufugaji kama ilivyoahidiwa na Serikali.

Akizungumza wakati wa mapokezi, Katibu Tarafa wa Sindeni, Bw. Baraka Nkatura, alisema Serikali imejipanga kuhakikisha kila mwananchi aliyekubali kuhama kwa hiari anapata huduma bora.
“Mtapatiwa nyumba za kisasa zilizojengwa kwenye maeneo yenye ukubwa wa ekari 2.5, mashamba ya ekari 5, na maeneo ya shughuli za ufugaji,” alisema Bw. Nkatura.

Miongoni mwa waliopokea nyumba mpya, Bw. Samweli Koromo alisema amefurahi kupewa nyumba bora na fursa za maendeleo ambazo hazikuwepo ndani ya hifadhi.
“Nimepata nyumba nzuri. Sasa nitaanza maandalizi ya kilimo kwa kuwa ni msimu wa mvua,” alisema.

Kwa upande wake, Bi. Esther Naftal, mkazi wa Msomera aliyehama Ngorongoro miaka mitatu iliyopita, alisema maisha yao yamebadilika kwa ubora.
“Msomera tunalima, tunafanya biashara, watoto wanasoma, na maisha yameimarika. Wito wangu kwa waliobaki Ngorongoro ni waendelee kujiandikisha ili wanufaike na fursa hii,” alisema.

Serikali kupitia Mamlaka ya Hifadhi ya Ngorongoro inaendelea kutoa elimu, kuandikisha, na kuhamisha wananchi wanaokubali kuhama kwa hiari. Ikielezwa kwamba wanaohama wanapewa uhuru wa kuchagua maeneo wanayotaka kuhamia huku Msomera ikiwa mojawapo ya maeneo yenye miundombinu bora.

Fuatilia @OrkonereiFM kwa habari zaidi kuhusu maendeleo ya zoezi hili.

Related Posts

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

Continue reading
Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
Enable Notifications OK No thanks