Matumizi ya Dawa Kiholela: Ni Tiba au Sumu?

Aliamka asubuhi akiwa na maumivu ya kichwa, Akaenda duka la dawa, akaeleza dalili, na kupewa dawa. Bila vipimo, bila ushauri wa daktari,Siku mbili baadaye hali yake ikawa mbaya zaidi. Hii si hadithi tu ila hii ni hali halisi ya maelfu ya Watanzania.

Bi. Fatuma Yusuph ni mmoja wa mashuhuda wa hatari ya matumizi ya dawa kiholela. “Nilijua ni malaria, nikameza dawa… kumbe haikuwa hivyo, Nilizidiwa,” anasema Fatuma.

Wataalamu wa afya wanazidi kutoa tahadhari, Mfamasia John Kazitanga anasema, “Dawa si kitu cha kufikiria kirahisi, lazima historia ya mgonjwa, dalili, na vipimo vijulikane” Vinginevyo, kinachodhaniwa kuwa tiba, kinaweza kuwa sumu.

Kwa mujibu wa utafiti wa Wizara ya Afya wa mwaka 2022, asilimia 59.8 ya Watanzania yaani takriban watu 6 kati ya kila 10 wanatumia dawa bila ushauri wa wataalamu. WHO inaongeza kuwa watu 700,000 hufariki kila mwaka duniani kutokana na usugu wa dawa – hali inayosababishwa kwa kiasi kikubwa na matumizi mabaya ya dawa.

Mganga Mfawidhi wa Zahanati ya Terrat, Tumaini Kamkama, anaeleza: “Ukitumia dawa kiholela, unaweza kuharibu ini, wengine wanaweza kupata madhara kwenye macho”

Wakazi wa vijijini mara nyingi hutegemea taarifa kutoka kwa marafiki, wauzaji wa maduka ya dawa au hata uzoefu wao wa zamani. “Ni ukiwa umechoka ama umemkosa daktari,” anasema mmoja.

Lakini dawa si chai Kuna wakati, kinachomezwa ni sumu ya polepole.

Kwa pamoja tunaweza kubadili hali hii. Elimu ya afya, ushauri sahihi, na huduma bora ndio suluhisho.

Je, dawa unazotumia ni tiba… au sumu?

  • Related Posts

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limefanya ukaguzi maalumu wa mabasi ya abiria ili kudhibiti ajali kutokana na ongezeko la wasafiri kipindi cha likizo za shule. Madereva wamehimizwa kuzingatia sheria…

    Continue reading
    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Zaidi ya madereva 800 wa magari ya utalii mkoani Arusha wamepatiwa mafunzo maalumu yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, ikiwa ni maandalizi ya msimu wa utalii (high…

    Continue reading

    One thought on “Matumizi ya Dawa Kiholela: Ni Tiba au Sumu?

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

    Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

    Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe

    Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe
    Enable Notifications OK No thanks