Marta Noah: Mwanamke wa Kimasai Aliyevuka Vikwazo Kumiliki Ardhi

Katika kijiji cha Loswaki, wilayani Simanjiro, Marta Noah ameandika historia ndogo lakini yenye ujumbe mkubwa. Katika jamii ya Kimasai ambako mila na desturi zimekuwa kizuizi kwa wanawake kumiliki ardhi, Martha ni miongoni mwa wachache waliothubutu na kufanikisha ndoto hiyo kupitia maelewano na mume wake.

Kupitia kipindi cha Nijuze cha Orkonerei FM Radio, Marta ameeleza jinsi alivyomwomba mume wake amtambue kwa kumpatia sehemu ya ardhi rasmi. Tangu mwaka 2019, baada ya kupata mtoto wao wa tatu, alikabidhiwa heka mbili ambazo amekuwa akizitumia kwa kilimo, ufugaji wa mbuzi na kuinua hali ya maisha ya familia.

“Nikaona nami nastahili kuwa na maendeleo yangu mwenyewe,” anasema Marta, ambaye sasa anamiliki mali binafsi ikiwemo mbuzi, meza, viti, na samani nyingine.

Mume wake anasema awali haikuwa rahisi, kutokana na mila, lakini aliona faida za usawa na maelewano ndani ya familia. “Maneno yapo,” anasema, “lakini niliona mazingira yetu. Sasa sina presha, yeye anajitegemea, hata watoto anawasaidia.”

Hadithi ya Marta ni mfano wa wazi wa mabadiliko yanayowezekana katika jamii za kifugaji kupitia elimu, upendo na ushirikiano wa familia.

  • Related Posts

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

    Continue reading
    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

    Continue reading

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
    Enable Notifications OK No thanks