HATUPIGI PICHA, TUNAPIGA SIMU: Changamoto za Mawasiliano Kijijini Sukuro

Je, umewahi kufikiria maisha ambayo kila unapohitaji kuwasiliana na familia yako, ni lazima upande juu ya mti ili upate mtandao?

Katika kijiji cha Sukuro, kilichopo kata ya Komolo, wilaya ya Simanjiro, mawasiliano ya simu si jambo rahisi. Kila siku, wananchi wa kijiji hiki wanapambana na changamoto ya mtandao hafifu wa simu, hali inayowalazimu kupanda juu ya miti ili kupiga simu au kutuma ujumbe. Katika sehemu nyingine, huduma za kutuma na kupokea pesa, ambazo zinahitaji mtandao, zimegeuka kuwa safari hatari, kwani wakala wa huduma hiyo hulazimika kupanda juu ya mti ili kuhudumia wateja wake.

Kwa wakazi wa Sukuro, mawasiliano yamekuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo na usalama. Wakazi, wanaelezea jinsi wanavyolazimika kutumia mbinu za kizamani na zenye hatari ili kufanikisha mawasiliano yao na ndugu zao walioko mbali.

https://www.instagram.com/reel/DA8BeY0PWDt/?utm_source=ig_web_copy_link&igsh=MzRlODBiNWFlZA==

Katika mazungumzo chini ya mti ambao ni sehemu pekee inayopatikana mtandao, wakazi wa kijiji hiki wameelezea hali yao kwa uchungu, wakionyesha matumaini ya kuwa siku moja, suluhisho la kudumu litapatikana. Mtendaji wa kijiji ameeleza hatua ambazo serikali ya kijiji imejaribu kuchukua ili kutafuta msaada wa kiteknolojia na kufanikisha upatikanaji wa mawasiliano ya uhakika kwa wananchi.

Related Posts

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limefanya ukaguzi maalumu wa mabasi ya abiria ili kudhibiti ajali kutokana na ongezeko la wasafiri kipindi cha likizo za shule. Madereva wamehimizwa kuzingatia sheria…

Continue reading
Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Zaidi ya madereva 800 wa magari ya utalii mkoani Arusha wamepatiwa mafunzo maalumu yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, ikiwa ni maandalizi ya msimu wa utalii (high…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe

Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe
Enable Notifications OK No thanks