HATUPIGI PICHA, TUNAPIGA SIMU: Changamoto za Mawasiliano Kijijini Sukuro

Je, umewahi kufikiria maisha ambayo kila unapohitaji kuwasiliana na familia yako, ni lazima upande juu ya mti ili upate mtandao?

Katika kijiji cha Sukuro, kilichopo kata ya Komolo, wilaya ya Simanjiro, mawasiliano ya simu si jambo rahisi. Kila siku, wananchi wa kijiji hiki wanapambana na changamoto ya mtandao hafifu wa simu, hali inayowalazimu kupanda juu ya miti ili kupiga simu au kutuma ujumbe. Katika sehemu nyingine, huduma za kutuma na kupokea pesa, ambazo zinahitaji mtandao, zimegeuka kuwa safari hatari, kwani wakala wa huduma hiyo hulazimika kupanda juu ya mti ili kuhudumia wateja wake.

Kwa wakazi wa Sukuro, mawasiliano yamekuwa kikwazo kikubwa cha maendeleo na usalama. Wakazi, wanaelezea jinsi wanavyolazimika kutumia mbinu za kizamani na zenye hatari ili kufanikisha mawasiliano yao na ndugu zao walioko mbali.

https://www.instagram.com/reel/DA8BeY0PWDt/?utm_source=ig_web_copy_link&igsh=MzRlODBiNWFlZA==

Katika mazungumzo chini ya mti ambao ni sehemu pekee inayopatikana mtandao, wakazi wa kijiji hiki wameelezea hali yao kwa uchungu, wakionyesha matumaini ya kuwa siku moja, suluhisho la kudumu litapatikana. Mtendaji wa kijiji ameeleza hatua ambazo serikali ya kijiji imejaribu kuchukua ili kutafuta msaada wa kiteknolojia na kufanikisha upatikanaji wa mawasiliano ya uhakika kwa wananchi.

Related Posts

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

Continue reading
Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
Enable Notifications OK No thanks