Wazazi wahimizwa kuwapeleka watoto wao shule

Wazazi wa Jamii ya Wafugaji wamaasai wametakiwa kutumia mifugo walionao na raslimali zingine kuwapeleka watoto wao Shule bila kuwabagua.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Shule ya Mchepuo wa Kiingereza ya Flaherty iliyopo Kijiji cha LoiborSoit A’ Kata ya Emboret Bw Altapuai Thadeus alipozungumza na Orkonerei FM Radio.

Bw Altapuai amesema kuwa ni vema jamii wakatambua kuwa elimu ndicho kitu muhimu na cha thamani kwa watoto wao hivyo ni vema wakawapeleka watoto shule pasipo kuwabagua.

Naye mkazi wa kijiji cha LoiborSoit A’ Bw Paulo Lenina amesema kuwa huu ni wakati ambao jamii ya wafugaji wanatakiwa wabadilike na kuwekeza kwenye elimu kwani misimu imekuwa ikibadilika na hata mataifa yalioendelelea wamefikia hatua hiyo baada ya kuelewa umuhimu wa elimu kwa kuwapeleka watoto wao shule.

Aidha Bw Paulo amesema kuwa kwa wakati huu wa mabadiliko ya tabianchi sio vema jamii ya wafugaji kuendelea kutegemea ufugaji wa mifugo wengi wasio na tija ila ni wakati wa kubadilisha mawazo kwa kuwekeza kwenye elimu kwa kuwapeleka watoto shule.

Shule ya Msingi Flaherty ni shule ya mchepuo wa kiingereza iliyopo kijiji cha LoiborSoit A’ kata ya Emboret wilayani Simanjiro na ni shule ya bweni na kutwa kwa wasichana na wavulana.

Mkurugenzi wa Shule ya Flaherty Altapuai Thadeus pamoja na Mkazi wa Kijiji cha LoiborSoit A’ Bw Paulo Lenina.

Related Posts

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

Serikali za vijiji katika Tarafa ya Terrat, wilayani Simanjiro, zimetakiwa kuwa na ushirikiano mzuri na wawekezaji waliopo kwenye maeneo yao kwa kuwaalika na kuwatembelea ili kujenga mahusiano mazuri na kushirikiana…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

Maji Safi na Salama ni Yapi?

Maji Safi na Salama ni Yapi?

Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja

Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja
Enable Notifications OK No thanks