Wazazi wahimizwa kuwapeleka watoto wao shule

Wazazi wa Jamii ya Wafugaji wamaasai wametakiwa kutumia mifugo walionao na raslimali zingine kuwapeleka watoto wao Shule bila kuwabagua.

Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Shule ya Mchepuo wa Kiingereza ya Flaherty iliyopo Kijiji cha LoiborSoit A’ Kata ya Emboret Bw Altapuai Thadeus alipozungumza na Orkonerei FM Radio.

Bw Altapuai amesema kuwa ni vema jamii wakatambua kuwa elimu ndicho kitu muhimu na cha thamani kwa watoto wao hivyo ni vema wakawapeleka watoto shule pasipo kuwabagua.

Naye mkazi wa kijiji cha LoiborSoit A’ Bw Paulo Lenina amesema kuwa huu ni wakati ambao jamii ya wafugaji wanatakiwa wabadilike na kuwekeza kwenye elimu kwani misimu imekuwa ikibadilika na hata mataifa yalioendelelea wamefikia hatua hiyo baada ya kuelewa umuhimu wa elimu kwa kuwapeleka watoto wao shule.

Aidha Bw Paulo amesema kuwa kwa wakati huu wa mabadiliko ya tabianchi sio vema jamii ya wafugaji kuendelea kutegemea ufugaji wa mifugo wengi wasio na tija ila ni wakati wa kubadilisha mawazo kwa kuwekeza kwenye elimu kwa kuwapeleka watoto shule.

Shule ya Msingi Flaherty ni shule ya mchepuo wa kiingereza iliyopo kijiji cha LoiborSoit A’ kata ya Emboret wilayani Simanjiro na ni shule ya bweni na kutwa kwa wasichana na wavulana.

Mkurugenzi wa Shule ya Flaherty Altapuai Thadeus pamoja na Mkazi wa Kijiji cha LoiborSoit A’ Bw Paulo Lenina.

Related Posts

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

Continue reading
Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
Enable Notifications OK No thanks