![pikipiki yenye madumu 10](https://ors-radio.co.tz/wp-content/uploads/2024/12/1733727832329.jpg)
#HABARI Wananchi wa kijiji cha Lorokare wameshiriki kueleza changamoto wanazokutana nazo, ikiwa ni pamoja na upotevu wa muda mwingi kufuata maji, hali inayowafanya wanawake wengi kushindwa kushiriki mikutano ya kijamii.
“Kukosekana kwa maji siyo tu kunatufanya tushindwe kuhudhuria mikutano, bali pia kumeathiri familia zetu, mpaka ndoa kuvunjika wakati wa kiangazi.”Mkaazi wa Lorokare
Viongozi wa kijiji wamesema kuwa wanahamasisha wananchi kuhudhuria mikutano, lakini changamoto ya maji imekuwa kikwazo kikubwa. Mwenyekiti wa kijiji, Bw. Alais Lukas Mollel, amesema wanahitaji msaada wa haraka ili kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa urahisi.
Sauti Kutoka kwa Wadau
Katika mahojiano na Diwani wa kata ya Oljoro No. 5, Bw. Loshie Lesakui, pamoja na Meneja wa RUWASA Wilaya ya Simanjiro, Injiniya Johanes Martin, tumepata maelezo kuhusu mikakati iliyopo kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi wa Lorokare. Meneja RUWASA amesema kuwa kuna matumaini makubwa ya kutatua changamoto hii kwa ushirikiano wa wadau wote.
Karibu kuisikiliza makala hii ya Nijuze Radio Show.