Unashiriki Vipi Mikutano ya Kijamii Kutatua Kero ya Maji?

#HABARI Wananchi wa kijiji cha Lorokare wameshiriki kueleza changamoto wanazokutana nazo, ikiwa ni pamoja na upotevu wa muda mwingi kufuata maji, hali inayowafanya wanawake wengi kushindwa kushiriki mikutano ya kijamii.

“Kukosekana kwa maji siyo tu kunatufanya tushindwe kuhudhuria mikutano, bali pia kumeathiri familia zetu, mpaka ndoa kuvunjika wakati wa kiangazi.”Mkaazi wa Lorokare

Viongozi wa kijiji wamesema kuwa wanahamasisha wananchi kuhudhuria mikutano, lakini changamoto ya maji imekuwa kikwazo kikubwa. Mwenyekiti wa kijiji, Bw. Alais Lukas Mollel, amesema wanahitaji msaada wa haraka ili kuhakikisha huduma ya maji inapatikana kwa urahisi.


Sauti Kutoka kwa Wadau

Katika mahojiano na Diwani wa kata ya Oljoro No. 5, Bw. Loshie Lesakui, pamoja na Meneja wa RUWASA Wilaya ya Simanjiro, Injiniya Johanes Martin, tumepata maelezo kuhusu mikakati iliyopo kuhakikisha huduma ya maji inawafikia wananchi wa Lorokare. Meneja RUWASA amesema kuwa kuna matumaini makubwa ya kutatua changamoto hii kwa ushirikiano wa wadau wote.

Karibu kuisikiliza makala hii ya Nijuze Radio Show.

Related Posts

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Malayoni,Malisho ya Mifugo na Hatari za Wanyamapori Orkonerei Fm Radio.Katika jamii ya Kimasai, vijana wa kiume huanza kuchunga mifugo kuanzia umri mdogo wa miaka mitano. Eneo la Ushoroba wa Kwakuchinja, lililopo Kata…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

Maji Safi na Salama ni Yapi?

Maji Safi na Salama ni Yapi?

Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja

Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja
Enable Notifications OK No thanks