WAZIRI MKUU AWATAKA WAHANDISI WAZINGATIE MAADILI

#Habari WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa awataka wahandisi wote nchini wazingatie miiko na maadili ya taalum hiyo ikiwemo kuitekeleza miradi ya ujenzi kwa ubora unaoendana na thamani ya fedha halisi iliyotolewa.

“Sote tunatambua kwamba wapo wachache katika taaluma yenu ya uhandisi ambao wanaichafua kwa kufanya matendo ambayo ni kinyume na taaluma lakini pia ni kinyume na maadili.” “Matendo hayo ni pamoja na rushwa, ubadhilifu, na ukosefu wa weledi. Hii si tu kwamba inachafua taaluma ya uhandisi, bali pia inaharibu taswira ya nchi”.

Ameyasena hayo leo (Desemba 06, 2024) kwenye Kongamano la Kimataifa la 14 la Taasisi ya Wahandisi Tanzania (IET), katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC), jijini Arusha.

Pia, Mheshimiwa Majaliwa ameiagiza Bodi ya usajili wa Wahandisi isimamie maadili ya kihandisi na makampuni ya kihandisi kwa mujibu wa sheria ili kulinda hadhi ya uhandisi nchini.

Waziri Mkuu ametoa rai kwa Taasisi ya Wahandisi Tanzania (IET) kuendelea kushirikiana na vyombo mbalimbali kuwabaini wanaokiuka maadili na sheria na kuchukua hatua stahiki kwani taaluma ya uhandisi ni muhimu na inapaswa kutunza na kulinda heshima yake.

Katika hatua nyingine, Mheshimiwa Majaliwa amezielekeza Mamlaka za Serikali za Mita na Usalama Barabarani kuhakikisha kuwa vizuizi na vituo vya ukaguzi vinazingatia usalama wa watumiaji na tahadhari zote za kiusalama.

“Wahandisi na wataalamu wetu mnao wajibu wa kuendelea kubuni na kupendekeza mifumo bora ya alama za barabarani, usimamizi wa miundombinu ya barabarana uwekaji wa vituo vya ukaguzi ili kupunguza ajali na madhara yake.”

  • Related Posts

    UMEME WALETA MAENDELEO KATA YA TERRAT, SIMANJIRO

    Nishati ya umeme imeleta mapinduzi makubwa ya maendeleo katika kata ya Terrat, mkoani Manyara. Wakazi wa eneo hili sasa wanashuhudia mabadiliko katika sekta mbalimbali, ikiwemo biashara, elimu, afya, na ajira,…

    Continue reading
    Mama Anayenufaika na Kilimo cha Mboga Msimu wa Kiangazi

    Katika kipindi cha kiangazi, wakazi wa Kijiji cha Terrat hukumbwa na changamoto ya upatikanaji wa mboga za majani. Hata hivyo, hali hii pia inatoa fursa kwa wakulima wabunifu wanaotumia mbinu…

    Continue reading

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

    Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

    Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe

    Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe
    Enable Notifications OK No thanks