RC Manyara Atembelea Vituo vya Watu Wenye Mahitaji Maalum Babati

Mkuu wa Mkoa wa Manyara, Mhe. Queen Cuthbert Sendiga, leo Disemba 29, 2024, ametembelea na kutoa zawadi za sikukuu ya mwaka mpya 2025 katika vituo vitatu vya watu wenye mahitaji maalum vilivyopo wilayani Babati. Vituo hivyo ni:

  1. Kituo cha Kulelea Wazee Magugu
  2. Kituo cha Kulelea Watoto Wenye Ulemavu Unaotibika cha Zilper
  3. Kituo cha Kulelea Watoto Yatima na Wanaoishi Mazingira Magumu cha Hossana

Zawadi hizo zimetolewa kwa niaba ya Mhe. Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kama ishara ya upendo wake kwa wananchi wanaoishi katika mazingira magumu wakati wa sikukuu hizi.

Mhe. RC Sendiga alieleza kuwa zawadi zilizotolewa, zenye thamani ya Shilingi Milioni 6.5, ni pamoja na:

  • Mchele
  • Mafuta ya kupikia
  • Sukari
  • Unga wa ngano
  • Viungo
  • Sabuni
  • Juisi
  • Maji
  • Mbuzi

Amesema kuwa zoezi la ugawaji zawadi linaendelea katika wilaya zote za Mkoa wa Manyara, lengo likiwa ni kuwafariji na kushirikiana na makundi maalum katika jamii.

Mkuu huyo wa Mkoa aliwahimiza wananchi kuendelea kuonyesha mshikamano, upendo, na kushirikiana na makundi haya maalum ili kudumisha mshikamano wa kijamii.

  • Related Posts

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    Serikali za vijiji katika Tarafa ya Terrat, wilayani Simanjiro, zimetakiwa kuwa na ushirikiano mzuri na wawekezaji waliopo kwenye maeneo yao kwa kuwaalika na kuwatembelea ili kujenga mahusiano mazuri na kushirikiana…

    Continue reading

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

    Maji Safi na Salama ni Yapi?

    Maji Safi na Salama ni Yapi?

    Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

    Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

    Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

    Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

    Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

    Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

    Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja

    Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja
    Enable Notifications OK No thanks