Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Zaidi ya madereva 800 wa magari ya utalii mkoani Arusha wamepatiwa mafunzo maalumu yaliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, ikiwa ni maandalizi ya msimu wa utalii (high season) unaotarajiwa kuanza hivi karibuni.

Akifungua mafunzo hayo, Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani nchini, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) William Mkonda, amesema mafunzo hayo yamelenga kuwakumbusha madereva sheria, kanuni na matumizi sahihi ya barabara ili kuhakikisha usalama wa watalii unaimarishwa, na hivyo kuitangaza vyema Tanzania kama taifa salama.

Aidha, Mwenyekiti wa Chama cha Waendesha Watalii nchini (TTGA), Bw. Lembrisi Moses, amesema kuwa madereva hao wamejengewa uwezo mkubwa kupitia mafunzo hayo, huku akieleza kuwa wamekumbushwa umuhimu wa kuzingatia alama za barabarani na mwendo sahihi.

Naye mmoja wa madereva walioshiriki mafunzo hayo, Bw. Usia Israel, amesema kupitia elimu hiyo wamejifunza kuhusu udereva wa kujihami ambao utasaidia kupunguza ajali za barabarani ambazo zinaweza kuepukika.

Mafunzo haya ni sehemu ya mkakati wa Jeshi la Polisi katika kuwajengea uwezo madereva wa makundi mbalimbali ili kuhakikisha usalama unatawala kwenye sekta ya utalii nchini.

Related Posts

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Jeshi la Polisi Mkoa wa Arusha limefanya ukaguzi maalumu wa mabasi ya abiria ili kudhibiti ajali kutokana na ongezeko la wasafiri kipindi cha likizo za shule. Madereva wamehimizwa kuzingatia sheria…

Continue reading
Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana mmoja aitwaye Joseph Gadiel mkazi wa kitongoji cha Kimelok, kijiji cha Ngiresi wilayani Arusha ameuawa kwa kuchomwa kisu baada ya kutokea ugomvi baina yake na kijana mwingine aliyetambulika kwa…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

Madereva wa Serikali Arusha Wawezeshwa kwa Mafunzo ya Usalama Barabarani

Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe

Wadau Waungana Kunusuru Mazingira ya Maasai Steppe
Enable Notifications OK No thanks