MGOGORO WA ARDHI WAPAMBA MOTO KATI YA TERRAT NA MWANANCHI

Mgogoro wa umiliki wa ardhi katika mpaka wa Kijiji cha Terrat, Kata ya Terrat, na Kijiji cha Sukuro, Kata ya Komolo, umeibua mjadala mkubwa katika mkutano mkuu wa kijiji cha Terrat uliofanyika Januari 13, 2024. Eneo lenye mgogoro linadaiwa kumilikiwa na mkazi wa Terrat, Bwana Marko Sangeti, huku serikali ya kijiji hicho ikisisitiza kuwa ni mali ya kijiji,Eneo likiwa ni zaidi ya hekari 200.

Katika mkutano huo, Bwana Marko Sangeti alisisitiza kuwa yeye ndiye mmiliki halali wa eneo hilo na akaeleza kuwa serikali ya kijiji inataka kumnyang’anya ardhi yake kwa madai kuwa ni mali ya kijiji.
“Ninamiliki eneo hili kihalali, na nina nyaraka zote zinazothibitisha. Tatizo ni kwamba mgogoro huu unachukuliwa kisiasa zaidi kila uchaguzi unapokaribia,” alisema Sangeti.

Historia ya Mgogoro
Aliyekuwa mwenyekiti wa kijiji cha Terrat miaka ya 1980, Bwana Isaya Nelukendo, alisema kuwa eneo hilo ni mali ya kijiji na si ya mtu binafsi.
“Tulipoweka mkataba tuliweka mkataba wa kijiji cha terrat wala siyo mtu mmoja,” alisema Nelukendo.

Isack Abraham, aliyekuwa mwakilishi wa kijiji cha Terrat wakati wa makabidhiano ya mkataba na taasisi inayomiliki ranchi ya Ormoti, aliunga mkono madai ya Bwana Sangeti. Aidha, Laigwanani Jacob Nduya, alifafanua mkataba huo, akisema kuwa ulikuwa na vipengele vinavyobainisha umiliki wa eneo hilo.

Mzozo Unavyoendelea
Mwenyekiti wa sasa wa kijiji cha Terrat, Ndg. Kone Medukenya, alisema kuwa mgogoro huo umekuwa ukijirudia mara kwa mara na unahitaji suluhisho la kudumu.
“Tulisema tuletee nyaraka ili tumalize huu mgogoro” alisema Medukenya.

Njia ya Suluhisho
Diwani wa Kata ya Terrat, Ndg. Jackson Matery, aliishauri serikali ya kijiji kuunda kamati ndogo ya kuchunguza umiliki wa eneo hilo na kutoa mapendekezo ya suluhisho.
“Naomba niombe kitu kimoja hatuwezi kumuambia Marko alete Documents hapa tuzisome mbele ya hadhara,” alisema Matery.

Mgogoro wa Kisiasa?
Bwana Sangeti aliongeza kuwa mgogoro huo unachochewa zaidi na siasa, hasa wakati wa uchaguzi.
“Kila wakati uchaguzi unapokaribia, ardhi yangu inageuka sehemu ya kampeni za kisiasa.” alisisitiza.

Mgogoro huu wa ardhi unaonyesha changamoto kubwa zinazokabili usimamizi wa rasilimali ardhi nchini Tanzania, hasa katika maeneo ya vijijini ambako mipaka ya ardhi haijabainishwa wazi.

Related Posts

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

Serikali za vijiji katika Tarafa ya Terrat, wilayani Simanjiro, zimetakiwa kuwa na ushirikiano mzuri na wawekezaji waliopo kwenye maeneo yao kwa kuwaalika na kuwatembelea ili kujenga mahusiano mazuri na kushirikiana…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

Maji Safi na Salama ni Yapi?

Maji Safi na Salama ni Yapi?

Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

Mbinu Bora za Uhifadhi wa Mazao ya Chakula kwa Usalama na Ufanisi

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Usalama wa Vijana Wanaochunga Mifugo Kwakuchinja

Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

Migogoro baina ya Wanyamapori na Binadamu Tanzania: Chanzo na Suluhisho

Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja

Namna Shule ya Msingi Burunge Inavyonufaika na Uhifadhi wa Ushoroba wa Kwakuchinja
Enable Notifications OK No thanks