TAWA Yasihi Serikali za Vijiji Kwenye Uhifadhi Kuimarisha Ujirani Mwema na Wawekezaji

Serikali za vijiji katika Tarafa ya Terrat, wilayani Simanjiro, zimetakiwa kuwa na ushirikiano mzuri na wawekezaji waliopo kwenye maeneo yao kwa kuwaalika na kuwatembelea ili kujenga mahusiano mazuri na kushirikiana katika maendeleo ya jamii.

Ushauri huo umetolewa na Afisa Mahusiano wa Mamlaka ya Usimamizi wa Wanyamapori Tanzania (TAWA) Simanjiro, Gabriel Charles, wakati wa kikao cha ujirani mwema kilichofanyika leo katika ofisi ya kata ya Terrat. Kikao hicho kilihusisha vijiji vya Tarafa ya Terrat vilivyopakana na maeneo ya hifadhi na vitalu vya uwindaji, na kiliongozwa na Afisa Tarafa Lekshon Kiruswa.

Umuhimu wa Kushirikiana na Wawekezaji

Katika kikao hicho, Bw. Charles alieleza kuwa kushirikiana na wawekezaji kwa njia ya mazungumzo na utembeleaji wa maeneo yao kunaweza kusaidia kupunguza changamoto zinazokumba vijiji husika, hasa katika sekta za afya na elimu.

“Kuwaalika ama kuwatembelea wawekezaji na kuwaeleza changamoto za vijiji husika kutasaidia kupunguza matatizo mbalimbali, lakini sisi kama TAWA hatuwezi kuwalazimisha wawekezaji kusaidia au kutosaidia,” alisema Bw. Charles.

Aidha, alifafanua kuwa michango inayotolewa na wawekezaji kwa jamii ni ya kisheria na hugawanywa kwa usawa kwa vijiji vilivyopo ndani ya maeneo ya uwekezaji.

“Kwa mfano, kuna mchango wa jamii wa dola 5,000 kwa kila muwekezaji, ambao ni wa kisheria na ni lazima utolewe. Kama muwekezaji hatimizi masharti hayo, basi hupewa nafasi mwingine,” aliongeza Bw. Charles.

Elimu kwa Viongozi na Wananchi Muhimu

Viongozi wa Vijiji Trafa ya Terrat

Kwa upande wake, Afisa Tarafa Lekshon Kiruswa alisisitiza umuhimu wa kuwa na kikao maalum kwa ajili ya kutoa elimu kwa wananchi na viongozi wa vijiji husika ili kuhakikisha ujirani mwema unadumishwa.

“Ni muhimu kuwa na semina maalum ili wananchi wapate uelewa wa kina kuhusu masuala haya. Pia ni vyema wawekezaji wawepo kwenye vikao hivi ili wajibu maswali yanayowahusu,” alisema Kiruswa.

Ushirikiano mzuri kati ya jamii na wawekezaji ni muhimu kwa maendeleo ya jamii na uhifadhi endelevu wa maliasili. Serikali za vijiji zinahimizwa kuchukua hatua za kujenga mahusiano mazuri na wawekezaji kwa manufaa ya jamii nzima.

Endelea kufuatilia tovuti yetu kwa taarifa zaidi kuhusu maendeleo ya jamii na uhifadhi wa maliasili katika Simanjiro na maeneo mengine.

Related Posts

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

Continue reading
Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
Enable Notifications OK No thanks