Wanawake na Utalii: Kongamano Kuu la Arusha 2025

Na Nyangusi Ole Sang’ida

Kongamano la Kanda ya Kaskazini kuelekea Siku ya Wanawake Duniani 2025 limefanyika mkoani Arusha, likihudhuriwa na Mgeni Rasmi, Mhe. Dkt. Stergomena L. Tax (MB), Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa. Kauli mbiu ya mwaka huu ni “Ushiriki wa Wanawake katika Utalii na Maliasili; Miaka 30 ya Azimio la Beijing.”

Dkt. Stergomena amepongeza hatua kubwa zilizofikiwa na Tanzania katika miaka mitatu tangu Azimio la Beijing, akisisitiza umuhimu wa kuendelea kutambua nafasi ya mwanamke katika jamii. Aidha, ameeleza kuwa juhudi za kuinua wanawake zimezaa matunda kwenye uongozi, uchumi, elimu, afya, na haki za binadamu.

Naibu Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Mwanaid Mwanahamis, amesema wizara imeratibu kongamano hili ili kuhakikisha kila mshiriki anapata fursa sawa, na kwamba wanawake sasa wanatambua nguvu zao – ndiyo maana wanaongoza katika nyanja mbalimbali.

Naye Jakiline Mafuru, Mwenyekiti wa Chama cha Wanawake Wenye Makampuni ya Utalii Tanzania, ameonesha furaha yake kwa ukuaji wa sekta ya utalii ambayo imewajumuisha wanawake madereva, wapokezi, na hata waongozaji watalii, hivyo kuchangia kwa kiasi kikubwa pato la taifa. Wajasiriamali walioshiriki kongamano hili wamesisitiza kuwa fursa hizo zinawafikia moja kwa moja, zikiwapa hamasa zaidi ya kupiga hatua mbele

  • Related Posts

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la madiwani jiji la Arusha limefungwa rasmi katika hafla ya kipekee iliyoongozwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa, Mh. Mohamed Mchechengerwa.…

    Continue reading
    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu…

    Continue reading

    Leave a Reply

    Your email address will not be published. Required fields are marked *

    You Missed

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Polisi Arusha Waimarisha Ukaguzi wa Mabasi Kukabiliana na Ajali

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Madereva 800 Wapatiwa Mafunzo Maalumu Kuelekea Msimu wa Utalii Arusha

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Kijana auawa kwa kisu Arusha, wananchi wachoma nyumba ya mtuhumiwa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa

    Jamii ya Maa Iwe Makini na Wanaotaka Kuigombanisha na Serikali – Fred Lowassa
    Enable Notifications OK No thanks