Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

World Sickle Cell Awareness Day ni siku inayoadhimishwa kila mwaka tarehe 19 Juni ili kuhamasisha elimu juu ya ugonjwa wa sikoseli. Ugonjwa huu wa damu, unaosababisha mabadiliko ya seli nyekundu za damu, unaathiri mamilioni ya watu duniani, hasa katika maeneo kama Tanzania.

Katika siku hii, jumuiya za afya, serikali na wadau hufanya kampeni za kuelimisha watu kuhusu ugonjwa huu, kuondoa ubaguzi, na kuongeza msaada kwa wagonjwa na familia zao.

Dkt. Fidelis Sunday wa Hospitali ya Mkoa wa Manyara anafafanua kuwa sikoseli ni ugonjwa unaosababisha seli za damu kuwa za umbo la sikio, kuziba mishipa ya damu na kusababisha maumivu makali, maambukizi na matatizo makubwa kiafya.

“Matibabu tunazotoa ni kuzuia maumivu, kuzuia damu kuganda na kuzuia maambukizi. Kuchelewa kupata matibabu kunaweza kusababisha matatizo makubwa kama kiharusi na hata kifo,” anasema Dkt. Fidelis.

Dkt. Fidelis anasisitiza umuhimu wa vipimo vya mapema:

“Wanandoa wanapaswa kufanya vipimo vya vinasaba kabla ya kuanza maisha ya ndoa ili kupunguza hatari kwa watoto wao.”

Kwa kuadhimisha siku hii, tunahimiza jamii kufahamu zaidi, kuhudhuria vituo vya afya, na kuhakikisha matibabu ya sikoseli yanapatikana kwa wote ili kuboresha maisha ya wagonjwa.

Related Posts

WWF-UK Wapongeza Juhudi za Wananchi wa Longido

Wawakilishi kutoka shirika la kimataifa la uhifadhi wa mazingira WWF-UK, Bi. Melanie na Bw. James, wametembelea kikundi cha wasikilizaji wa redio katika wilaya ya Longido kinachonufaika na mradi wa REDAA…

Continue reading
KINNAPA Yarejesha Wasichana 200 Mashuleni Manyara

Shirika lisilo la kiserikali la KINNAPA Tanzania, limefanikiwa kurejesha zaidi ya wanafunzi 200, hasa wasichana, mashuleni katika wilaya za Simanjiro, Kiteto, Babati, Siha na Hai, kupitia mradi wake wa “Mpe…

Continue reading

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

You Missed

Embooreet Sekondari Yageuza Kinyesi Kuwa Nishati Safi ya Kupikia

Embooreet Sekondari Yageuza Kinyesi Kuwa Nishati Safi ya Kupikia

WWF-UK Wapongeza Juhudi za Wananchi wa Longido

WWF-UK Wapongeza Juhudi za Wananchi wa Longido

KINNAPA Yarejesha Wasichana 200 Mashuleni Manyara

KINNAPA Yarejesha Wasichana 200 Mashuleni Manyara

Simanjiro: Watu Wenye Ulemavu na Ushiriki wa mikutano ya maamuzi

Simanjiro: Watu Wenye Ulemavu na Ushiriki wa mikutano ya maamuzi

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Baraza la Madiwani Arusha Laitimishwa Rasmi, Viongozi Wasisitiza amani

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii

Siku ya Elimu ya Ugonjwa wa Sikoseli Duniani — 19 Juni: Kuleta Mwanga kwa Wagonjwa na Jamii
Enable Notifications OK No thanks